Kilio cha Familia Bungoma Podcast Por  arte de portada

Kilio cha Familia Bungoma

Kilio cha Familia Bungoma

Escúchala gratis

Ver detalles del espectáculo

Famili moja kutoka eneo la Ndengelwa kaunti ya Bungoma sasa imeitaka serikali ya Kenya na ile Canada kuingilia kati na kuwasaidia ili wakaweze kusafirisha mwili wa mpendwa wao na kumzika nyumbani kwao katika kijiji cha Ndengelwa.Elizabeth Nekesa ambaye ni mamake marehemu anadai kuwa Leonard Wandili aliyesafiri nchini Canada kikazi alifariki akiwa huko huku familia yake ikikosa kujua kiini cha kifo cha mpendwa wao .

“Niliachana na mtoto wangu tarehe mbili akiwa mzima, naomba mwili ufanyiwe upasuaji ili nielezwe mwanangu alikufa kivipi,mtoto alienda huko kikazi ,wanisaidie mwili wa mtoto wangu urudi kenya”…


Kwa sasa familia hiyo imeitaka serikali hizi mbili kuwasaidia ili wakaweze kujua kiini cha kifo cha mpendwa wao na mwili wake kusafirishwa nchini Kenya ili akaweze kuzikwa na familia yake kulingana na desturi na mila za jamii ya Bukusu.

Todavía no hay opiniones